• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Mradi wa zaidi ya Bilioni 40 kuchagiza mapambano ya Malaria Katavi, Katibu Tawala Katavi awataka Wataalamu wa Afya kuleta matokeo chanya .

Posted on: September 12th, 2022

Taasisi ya Afya Ifakara (IHI) katika jitihada zake za kupambana na Ugonjwa wa Malaria Nchini   imeutambulisha Mradi wa miaka 5 utakaosaidia mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria Mkoani Katavi.

Akiutambulisha Mradi huo katika ukumbi wa Katavi Resort Manispaa ya Mpanda Mwakilishi kutoka Taasisi ya Afya Ifakara Dkt.Dustan Bishanga ameeleza kuwa Mradi huo unaojulikana kama Malaria Survailance Activity unafadhiliwa na Shirika la USAID kupitia mfuko wa Rais wa Marekani wa kupambana na Malaria PMI (President Malaria Initiative) ambapo zaidi ya Bilioni 40 zitatolewa na Mfuko huo kwa ajili kutelekeza Mradi huo.

Dkt.Bishanga amesema Mradi huo utajikita zaidi katika Uboreshaji wa huduma za Malaria,Kujenga uwezo kwa watumishi wa wanaohusika na utoaji wa huduma za Ugonjwa Malaria,Utoaji wa Elimu kwa Wananchi pamoja na Uimarishaji mifumo ya Taarifa za  Ugonjwa Malaria itakayosaidia kujua mwenendo wa Ugonjwa wa Malaria Mkoani Katavi.

Akizungumza katika kikao cha Utambulisho wa Mradi huo  Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Bw.Hassan Abas Rugwa amesema Mradi huo umekuja kwa wakati muafaka kwa kuwa Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa yenye kiwango cha juu cha maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria kwa Asilimia 7.1

Katibu Tawala Rugwa amesema ni muhimu kwa Wataalamu wa Afya pamoja na wadau wote katika Mapambano ya Malaria kuelekeza jitihada kubwa katika kuhakikisha kuwa mradi uliotambulishwa unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa ili uweze kuleta matokeo chanya ya kuondoa Malaria jambo litakalosaidia kuchochea ukuaji wa Uchumi Mkoani Katavi.

Bw.Rugwa ameeleza kuwa uwepo wa Ugonjwa wa Malaria kunachangia kwa kiasi kikubwa kuathiri uchumi katika Sekta mbalimbali Nchini ikiwemo sekta ya Utalii kwa kuwa Watalii wengi hawapendelei kutembelea maeneo ambayo yametajwa kuwa na kiwango cha juu cha maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria.

Aidha Katibu Tawala Rugwa ametoa wito kwa wataalamu wa Afya Mkoani Katavi kuendelea kutoa elimu ya kutosha kwa Wananchi juu ya njia mbalimbali za kupambana na Malaria ikiwemo Matumizi ya Vyandarua,Usafi wa Mazingira,Matumizi ya Viuadudu, pamoja na kuhamasisha matumizi ya Teknolojia ya kisasa ya matumizi ya Vifaa vya kielektroniki vya kuangamiza Mbu.

Kwa Upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bw.Omari Sukari ameishukuru Taasisi ya Afya Ifakara kwa kusapoti mapambano ya malaria Mkoani Katavi

Ameeleza kuwa licha ya jitihada mbalimbali za Serikali kupambana  na malaria  bado maambukizi ya ugonjwa wa malaria yamekua yakiongezeka ambapo kwa sasa bado kama Mkoa wanaendelea na jitihada za Ugawaji wa Vyandarua pamoja na utoaji wa Elimu ya namna ya kutokomeza malaria husuani kwa watoto chini ya Umri wa miaka 5 pamoja na Akina mama wajawazito.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Mpanda Bi Sofia Kumbuli ameishukuru Taasisi ya Afya Ifakara kwa kutoa sapoti kubwa itakayosaidia kwa sehemu kubwa mapambano ya Malaria Mkoani Katavi ambapo kwa niaba ya Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Katavi ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza mradi huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved