• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MRADI WA BEVAC WABORESHA SEKTA YA UFUGAJI NYUKI MKOANI KATAVI.

Posted on: July 9th, 2025

Mratibu wa Mradi wa BEVAC, Bi. Flosia Vugo, kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, wamefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kutembelea Chama cha Ushirika cha Mazao ya Nyuki na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha usindikaji wa mazao ya nyuki. Kituo hicho kinatarajiwa kuwa nguzo muhimu ya kuongeza thamani ya mazao kama asali na nta, na kuchangia katika kuimarisha uchumi wa wakazi wa eneo hilo. Katika ziara hiyo, jumla ya ndoo 270 zilikabidhiwa kwa chama hicho ili kusaidia shughuli za uvunaji wa asali kwa kutumia njia bora na za kisasa.


Timu hiyo pia ilitembelea eneo la “Manzuki Darasa” ambalo limeandaliwa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wafugaji wa nyuki. Kupitia darasa hilo, wanakikundi hujifunza mbinu bora za ufugaji wa nyuki, utunzaji wa mizinga, na usindikaji wa mazao ya nyuki kwa kuzingatia viwango vya ubora.

Katika hatua nyingine, timu hiyo ilitembelea Kikundi cha Wasakatonge kilichopo Kata ya Sibwesa, ambacho kina jumla ya wanachama 17. Kikundi hicho kilikabidhiwa mizinga 57 ya kisasa, ikiwa ni juhudi za kuongeza uzalishaji wa asali na kuimarisha kipato cha wanakikundi. Hata hivyo, kikundi hicho kilibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri utekelezaji wa shughuli zao, ikiwemo upungufu wa mavazi ya kinga kwa ajili ya kuvuna asali na ukosefu wa mashine ya kisasa ya kukamulia asali.

Afisa Mifugo wa Mkoa wa Katavi, Bw. Zidihery Mhando, aliwahimiza wanakikundi kutumia vyema fursa zinazotolewa na mradi huo kwa lengo la kukuza uzalishaji na kuongeza thamani ya mazao ya nyuki. Alisisitiza kuwa sekta ya ufugaji wa nyuki ni mojawapo ya maeneo yenye fursa kubwa ya kiuchumi, hasa kwa vijana na wanawake, na kwamba ushiriki wao kikamilifu katika miradi kama hii utaleta mabadiliko ya kweli ya kiuchumi na kijamii.

Mradi wa BEVAC unaendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa wafugaji wa nyuki kwa kuwajengea uwezo wa kuzalisha kwa wingi, kuchakata kwa ubora, na kuuza mazao yao kwa faida, hivyo kuchangia kikamilifu katika kukuza uchumi wa kaya na taifa kwa ujumla.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SEPTEMBA 2025, MWISHO WA MATUMIZI YA MKAA NA KUNI KWENYE TAASISI ZINAZO HUDUMIA WATU ZAIDI YA 100. HUDUMIA

    July 23, 2025
  • KATAVI YAANZA KUYABAINISHA MAENEO HATARISHI YANAYOCHOCHEA MAGONJWA YA MLIPUKO.

    July 22, 2025
  • HUDUMA YA KUCHUJA DAMU (DIALYSIS): TUMAINI JIPYA KWA WAGONJWA WA FIGO KATAVI.

    July 21, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUTUMIA MADHABAHU KUKEMEA NA KUELIMISHA UMMA JUU YA MADHARA YA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI.

    July 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved