• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Maafisa Ugani/Mifugo watakiwa kutoa elimu ya Ufugaji kwa walengwa wa TASAF

Posted on: July 1st, 2022

Pichani:Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe.Bi Jamila Yusuph Kimaro alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko katika Ufunguzi wa Kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa TASAF kilichoketi katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda 30 Juni 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe.Jamila Yusuph Kimaro amewaelekeza  Wakurugenzi wa Halmashuri paomja na Maafisa Ugani wa Halmashauri  kuwajengea uwezo Walengwa katika Mpango wa kunusuru kaya Maskini wa TASAF waweze kutumia mbinu bora na za kisasa za ufugaji ili waweze kutumia Elimu hiyo kuendeleza miradi mbalimbali wanayoianzisha.

Mhe Kimaro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko,  ametoa maelekezo hayo alipofungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF Mkoani katavi kilichoketi  katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Mpanda kujadili namna ambavyo mpango huo umetekelezwa kwa kipindi cha Mwaka Mzima.

Ameeleza kuwa iwapo walengwa katika mpango wa kunusuru Kaya masikini wa TASAF watejengewa uwezo na kupewa elimu ya mbinu bora na za kisasa za ufugaji itawasaidia kwa sehemu kubwa kutumia ruzuku wanazozipata kupitia mpango huo kujikwamua na umasikini na hatimae kufikia azma ya Serikali ya kuwaondolewa Umasikini.

Aidha Mhe.Mkuu wa Wilaya huyo amewasisitiza Waratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Nchini TASAF Mkoani Katavi kujipanga kuhakikisha kuwa taarifa za walengwa zinapatikana na kuwasilishwa kwa wakati ili kuondoa malalamiko katika ngazi ya Jamii.

Amewapongeza Waratibu na wasimamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Nchini Mkoani Katavi kwa kuhakikisha kuwa Mpango huo unaendelea kutekelezwa na kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Katavi Bi.Anna Shumbi  amesema kuwa kupitia tathmini iliyofanyika imebaini kuwa Mpango wa TASAF umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuimarisha na kuboresha upatikanaji wa  huduma mbalimbali kwa walengwa.

Ameeleza kuwa kupitia Mpango wa TASAF Walengwa katika mpango huo wamefanikiwa kuwapeleka watoto wao Mashuleni ambapo kupitia ruzuku wanazopata zimewasaidia kuhakikisha kuwa Watoto walioko mashuleni chini ya Mpango huo wanapatiwa mahitaji muhimu kama vile Sare,Madaftari pamoja na mahitaji mengine ya Shule.

Mpango wa TASAF pia umefanikisha upatikanaji wa huduma bora za Afya kwa walengwa ambapo walengwa katika moango huo wamefanikiwa kujiunga na CHF iliyoboreshwa jambo linalowahakikishia uhakika wa matibabu pindi wanapougua ameeleza Bi.Shumbi

Ameeza pia kuwa Walengwa kupitia mpango wa Kunusuru Kya Maskini TASAF Mkoani Katavi  wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katik ujenzi wa nyumbaa za gharama nafuu ukilinganisha na nyumba ambazo walikuwa wakiishi kabla hawajaingia katika Mpango.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved