• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Wafanyakazi Katavi waaswa kujiepusha na Rushwa,Wahimizwa kuchapa kazi kuleta Maendeleo.

Posted on: May 1st, 2022

Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Mei Mosi 2022, Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mh.Filberto Sanga(Aliyevalia Suti Katikati) kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi akipokea maelezo kuhusu namna  ya kurekebisha Mfumo wa Gurudumu za Gari  kwa kutumia Mfumo wa Kompyuta kutoka kwa Mkufunzi  wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA-Mpanda alipotembelea Banda la maonyesho katika maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Mei Mosi 2022 yaliyofanyika katika Uwanja wa  Kashaulili  Manispaa ya Mpanda.


Na: John Mganga-IO-Katavi RS

Wafanyakazi kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yakiwemo mashirika pamoja na Taasisi  Binafsi Mkoani Katavi wameungana na Wafanyakazi wenzao kote Nchini na Duniani kwa Ujumla  kuadhimisha Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani Mei mosi.

Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo,Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mh.Filberto Sanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh.Mwanamvua Mrindoko ameongoza Wafanyakazi katika kusherehekea Siku hiyo muhimu ya Wafanyakazi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mh.Sanga ametoa wito kwa Wafanyakazi Mkoani Katavi kuongeza bidii katika kutekeleza majukumu yao kikamilifu pamoja na kuzingatia Sheria kanuni na Taratibu za Ajira ili kuliletea Taifa maendeleo.

Ameeleza kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa wa Wafanyakazi katika Sekta mbalimbali Nchini  na kwamba itaendelea kuhakikisha kuwa inasimamia na kulinda maslahi mapana ya Wafanyakazi pamoja na kuboresha stahiki mbalimbali kwa wafanyakazi ili waweze kuleta tija iliyokusudiwa.

Mh.Sanga amewataka Watumishi wa Umma ambao wamekabidhiwa dhamana kubwa ya kutoa huduma kwa Wananchi  kujihadhari na tabia na vitendo  mbalimbali vinavyoshusha hadhi ya Watumishi wa Umma jambo linaloichafua Serikali.

Amezitaja tabia hizo kuwa ni pamoja na Lugha chafu wakati wa kuhudumia Wananchi,tabia mbaya ya kuomba rushwa ambapo amesisitiza kuwa Serikali haitosita kuchukua hatua a kinidhamu kwa wale wote watakaobainika kuendeleza vitendo hicyo visivyokubalika katika Jamii.

Awali katika Risala ya Wafanyakazi iliyosomwa na uwakilishi kutoka vyama vya Wafanyakazi Mkoani Katavi imeelezwa kuwa watumishi bado wanakabiliwa na changamotyo mbsalimbali jambo linaloathiri kwa sehemu kubwa Utendaji kazi kwa watumishi wa Umma

Aidha wafanyakazi wameiomba serikali kuborsha kuendelea kuboresha maslahi mbalimbali kusudi kuleta tija katika utumishi wa Umma.

Katika Maadhimisho hayo yanayofanyika kila Mwaka Mh.Sanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh.Mwanamvua Hozza Mrindoko amekabidhi Zawadi mbalimbali kwa Wafanyakazi kutoka Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi ili kuamsha ari kwa Wafanyakazi

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved