• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Katibu Tawala Katavi awataka Watumishi Tanganyika kudumisha mahusiao mema kazini.

Posted on: September 5th, 2022

Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Bw.Hassan Abas Rugwa amewaasa watumishi Wilayani Tanganyika kudumisha ushirikiano na mahusiano mema kazini ili kufikia malengo mahsusi ya Serikali ya utoaji huduma bora kwa Wananchi.

Katibu Tawala Rugwa ametoa rai hiyo alipozungumza na Watumishi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Tanganyika katika ziara yake Wilayani humo Septemba 5, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika,ikiwa ni sehemu ya ratiba yake kukutana na kuzungumza na watumishi wa kada mbalimbali Mkoani Katavi kwa lengo la kujitambulisha ikiwa ni muda mchache tangu kuwasili Katavi akitokea Kituo chake cha awali Dar Es Salaam.

Bw.Rugwa amewaambia watumishi wa Tanganyika  kuwa kutokana na Watumishi wa Umma kutumia muda mwingi mahala pa kazi kuliko maeneo mengine ni muhimu kudumisha mahusiano mazuri kazini kwa kupendana na kuthaminiana  ili kuboresha mazingira ya kazi jambo ambalo litasaidia kwa sehemu kubwa kufikia malengo mahsusi ya Serikali ya utoaji wa huduma bora kwa Wananchi.

Katibu Tawala Rugwa ameahidi ushirikiano wa kutosha kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika akiwataka kutosita kufika ofisini kwake iwapo kuna changamoto yoyote ya kiutumishi inayowakabili watumishi hao.

Aidha Bw.Rugwa ameongeza kuwa ni furaha yake kuona watumishi wa Umma  Mkoani humo wanapiga hatua kimaendeleo na kufikia malengo yao jambo ambalo linaleta Afya katika utumishi wa Umma.

“Kwa hiyo mimi matarajio yangu ni kuwa licha ya kuwa kiongozi naahidi kuwa mlezi mzuri wa watumishi,Katavi ni sehemu nzuri sana ya Watumishi kufikia matarajio yao”

Katibu Twala Rugwa pia ameongeza kuwa Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa Nchini inayokua kwa kasi zaidi ukilinganisha na mikoa mingine iliyoanzishwa miaka ya karibuni hivyo ni vema Watumishi wakatizama fursa za kuchumi zilizopo na kuzitumia ili kufikia malengo mahsusi ya kujiletea maendeleo.

Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Bw.Betuely Ruhega ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika licha ya mafanikio makubwa iliyoyapata bado   inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi pamoja na Vitendea kazi ambapo amemuahidi Katibu Tawala Mkoa kuwa wanaendelea na jitihada za kutatua changamoto hizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UTOAJI HAKI.

    May 28, 2025
  • RC MRINDOKO AKEMEA WAKURUGENZI KUZALISHA MADENI MAPYA KWA WAZABUNI.

    May 22, 2025
  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

    May 20, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved