• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Katavi washiriki maonyesho ya Nanenane Mbeya.

Posted on: August 3rd, 2022

Pichani:Wananchi mbalimbali wakipewa Elimu kuhusu ufugaji wa Kisasa wa Samaki katika Mabwawa katika banda la Maonyesho la Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika katika Viwanja vya John Makangare yanayoendelea Jijijini Mbeya.


Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa 7 ya Nyanda za Juu kusini inayoshiriki kikamilifu katika maonyesho ya bidhaa za Kilimo Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya John Mwakangare Jijijini Mbeya.

Maonyesho hayo yaliyozinduliwa rasmi 1 Agosti 2022 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango yanaendelea kuupamba mji wa Mbeya ikiwa ni Siku ya tatu tangu kuzinduliwa kwake.

Jumla ya Halmashauri tano  za Mkoa wa Katavi ambazo ni  Manispaa ya Mpanda,Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika,Mpimbwe,Mlele na Nsimbo zinashiriki kikamilifu katika maonyesho hayo ambapo Wajasiriamali  wasindikaji wa bidhaa mbalimbali,Wafugaji na Wakulima wamepata fursa ya kushiriki katika maonyesho hayo kwa ajili ya kuonyesha bidhaa mbalimbali zinazozalishwa katika Mkoa wa Katavi.

Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi amesema  maonyesho hayo yanatoa fursa kwa Wakulima,Wafugaji na Wajasiriamali kuonyesha bidhaa mbalimbali zinazozalishwa kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambapo ametoa Rai kwa Wananchi mbalimbali kutembelea Banda  la Maonyesho la Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa ajili ya kujifunza mbinu bora na za kisasa za Kilimo cha Mazao mbalimbali pamoja na kujifunza shughuli mbalimbali za ufugaji pamoja na Ujasiriamali wa bidhaa mbalimbali

Abdala Kakoso Mjasiriamali na mfugaji Nyuki kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika amewataka Wananchi kufika katika Banda la Halmashauri ya WilayaTanganyika kujionea mazao mbalimbali ya Nyuki pamoja na kujifunza faida mbalimbali zitokanazo na mazao ya Nyuki.

Naye Mstahiki Mea wa Manispaa ya Mpanda Mhe.Haidary Sumry ameeleza kuwa kama Manispaa ya Mpanda imejipanga kuhakikisha kuwa inashiriki kikamailifu katika manyesho hayo huku akiahidi kuwa Mansipaa hiyo itaibuka Mshindi katika Maonyesho hayo ya Nanenane Kikanda Mkoani Mbeya.

Mfugaji wa N,gombe wa Kisasa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Bw.Jamal Nasor Mahmoud amesema  ni muhimu kwa Wananchi wanaoshiriki katika maonyesho hayo ya Bidhaa za Kilimo nanenane  kujifunza zaidi kuhusu ufugaji wa Kisasa wa N,gombe katika banda la Manispaa ya Mpanda na  kuachana na N,gombe wa kienyeji kwa kuwa ngombe wa kisasa wana faida kubwa ukilinganisha na ngombe wa Kienyeji ambao kwa wakati huu hawana tija.

Maonyesho ya bidhaa za Kilimo nanenane yataendelea hadi siku ya Kilele chake Tarehe 8 Agosti 2022 ambapo Mgeni rasmi katika Kilele cha Maonyesho hayom anatarajiwa kuwa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved