• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

KAIMU KATIBU TAWALA WA MKOA WA KATAVI AHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA USALAMA WA MTOTO MTANDAONI.

Posted on: March 26th, 2025

Katavi, Machi 26, 2025


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Florence Chrisant, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa watendaji wa Serikali katika kuhakikisha mafanikio ya programu ya usalama wa mtoto mtandaoni.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni, Bw. Chrisant amesema kuwa licha ya Serikali kuanzisha programu mbalimbali za kusaidia wananchi, changamoto ya ukosefu wa ushirikiano imeathiri utekelezaji wake.

“Kila mmoja anapaswa kuwajibika kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya madhara ya mitandao ya kijamii,” amesema Bw. Chrisant huku akiongeza kuwa matumizi mabaya ya mtandao yamechangia mmomonyoko wa maadili kwa watoto na vijana.

Amehimiza wazazi kuwa karibu na watoto wao, kuwapa mwongozo sahihi katika matumizi ya teknolojia, na kuhakikisha wanatumia mitandao kwa malengo chanya.

Kwa upande wake, Mtaalamu wa Usalama Mtandaoni, Bw. Yusuph Kileo, amesema tafiti zinaonyesha kuwa asilimia 87 ya mitandao ya kijamii inachangia mmomonyoko wa maadili. Amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua za kulinda watoto dhidi ya ukatili wa mtandaoni kupitia programu hiyo.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bi. Mwelinde Katto, amesema kampeni hii inalenga kutoa elimu kwa watoto, wazazi, walimu, na jamii kwa ujumla kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni. Ameeleza kuwa tafiti zinaonyesha kuwa asilimia 67 ya watoto wenye umri wa miaka 12 hadi 17 wanatumia mitandao ya kijamii, huku asilimia 5 wakilazimishwa kutuma picha zisizofaa.

Mafunzo hayo yamewaleta pamoja wataalamu wa Maendeleo ya Jamii, Maafisa Ustawi wa Jamii, Wakuu wa Dawati la Jinsia la Polisi, na mashirika yasiyo ya kiserikali kutoka mikoa ya Katavi, Rukwa, na Tabora.

Akihitimisha, Bw. Chrisant ameipongeza Wizara ya Maendeleo ya Jamii kwa kuanzisha programu hiyo, akitoa wito kwa wadau wote kushiriki kikamilifu katika kulinda watoto dhidi ya hatari za mtandaoni.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved