• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Halmashauri Katavi zapongezwa kuvuka malengo ukusanyaji wa mapato.

Posted on: August 17th, 2022

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akimtunuku cheti cha Mshindi wa kwanza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Bi.Theresia Irafay kwa kuibuka kidedea katika ukusanyaji wa mapato Mwaka wa fedha 2021/2022 katikaUkumbi wa Maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ulioko  Manispaa ya Mpanda.

Mpanda.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko amezipongeza Halmashauri na Taasisi mbalimbali mkoani   humo kwa kufanikisha Mkoa  huo kufikia  na kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Mhe.Mrindoko ametoa pongezi  hizo  16 Agosti 2022  katika kikao cha Tahmini ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti  ya Mkoa  kilichokutanisha Taasisi  mbalimbali za Serikali Mkoani humo kwa lengo la kutathmini utekeleaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2021/2022 katika ukumbi wa Maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Mhe.Mrindoko amezitaka Halmashauri Mkoani Katavi pamoja na Taasisi mbalimbali zinazohusika katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali  kutobweteka kwa pongezi na badala yake kuongeza juhudi zaidi za ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Akiwasilisha Taarifa ya tahmini  ya mapato ya ndani ya Halmashauri  kimkoa Katibu tawala msaidizi sehemu ya usimamizi wa Serikali za Mitaa Bw.Florence Crisant ameeleza kuwa hadi kufikia 30 Juni 2022 Halmashauri za Mkoa wa Katavi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 zilikuwa zimekusanya jumla ya Shilingi Bilioni 13.6 sawa na Asilimia 112 ya Makisio ya shillingi Bilioni 12.1.

Taarifa hiyo imezitaja Halmashauri 3 kati ya 5 za Mkoa wa Katavi kuvuka Malengo ya ukusanyaji ikiongozwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mlele ambayo imekusanya shilingi 1, 774,087,421 sawa na Asilimia 185 ikivuka lengo lake la mwaka la makusanyo ya Shilingi 957,000,000 katika mwaka wa fedha 2021/2022.

Halmashauri zingine zilizovuka malengo ya ukusanyaji wa mapato ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe ambayo imefanikiwa kuvuka lengo la makusanyanyo ya mwaka ya Shilingi 1,973,554,176 kwa kukusanya Shilingi 2,540,837,091 sawa na asilimia 129 ikishika nafasi ya Pili huku Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ikivuka malengo ya mwaka wa fedha 2021/2022 ya Shilingi 1,191,000,000 na kukusanya Shilingi 1,421,815,380 ikishika nafasi ya tatu.

Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imeshika nafasi ya nne ikitembea ndani ya makisio yake kwa kukusanya Shilingi 4,452,617,530 sawa na Asilimia 100 ikifuatiwa na Manispaa ya Mpanda nafasi ya tano ambayo imekusanya Asilimia 97 ya Makisio ya Shilingi 3,577,000,000.

Aidha katika Kikao hicho Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoani Katavi pia  katika Taarifa yake ilionyesha kuvuka lengo kwa ongezeko la Asilimia 32 kwa kukusanya  zaidi ya Shilingi Bilioni 8 kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Kwa upande wa Sekta ya Madini Ofisi ya Afisa Madini Mkazi katika taarifa yake ilionyesha kuvuka malengo ya ukusanyaji kwa kukusanya Shilingi 6, 256, 198, 091.67 sawa na  Asilimia 131.71 ukilinganisha na lengo la mwaka la makusanyo ya Shilingi Bil.4.75.


Picha 2.Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akimtunuku Cheti Bi.Catherine Mashalla,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa kuibuka mshindi wa pili katika ukusanyaji wa Mapato Kimkoa 16 Agosti 2022 katika ukumbi wa Maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganhyika ulioko Manispaa ya Mpanda.



Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akimtunuku cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani kwa kuibuka Mshindi wa tatu kimkoa katika ukusanyaji wa mapato.



Mkuu wa Mkoa wa Katavi akimtunuku cheti Meneja wa TRA mkoa wa  Katavi.Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Katavi nao ni miongoni mwa Taasisi zilizovuka malengo ya ukusanyaji wa Mapato Mkoani Katavi




Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Katavi akitunukiwa zawadi ya cheti kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Katavi kwa kuvuka mlengo ya ukusanyaji wa Mapato.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved