• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

HALI YA LISHE

Posted on: September 12th, 2017

WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI WATAKIWA KUZINGATIA MASUALA YA LISHE

Bi.Asnath Mrema Afisa Lishe Mkoa wa Katavi akiongea na walengwa wa Mpango wa TASAF Mkoa wa Katavi amesema kuwa Mkoa wa Katavi bado haufanyi vizuri sana katika suala zima la lishe, hali ambayo inachangia kuwa na athari nyingi zinazotokana na hali ya lishe moja kwa moja au zinazochangia kuwepo na matatizo mengine ya kiafya kwa jamii ya wanakatavi kwa ujumla wake.

Bi.Asnath amesema kuwa pamoja na kuwa Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa Mikoa inayozalisha chakula kwa wingi bado Mkoa unakabiliwa na tatizo kubwa la lishe kwa wananchi wake. Lishe duni ni moja ya matatizo makubwa ya kiafya yanayoathiri haswa watoto wadogo, wachanga na wanawake walio katika umri wa kuzaa nchini. Kwa watoto chini ya miaka 5 tafiti zinaonyesha kuwa hali ya udumavu katika Mkoa wa Katavi ni asilimia 39 ukilinganisha na asilimia 34 kitaifa. Uzito pungufu ni asilimia 15.4 kwa Mkoa wa Katavi na kitaifa ni asilimia 14.0. Upungufu wa damu  ni asilimia 54.9 kimkoa na Kitaifa  ni asilimia 57. Bi.Asnath amesema kuwa moja ya changamoto  inayowakabili wanawake wenye umri wa miaka 15 – 49 ni upungufu wa damu ambapo kati ya wanawake kumi (10) watano (5) wanaupungufu wa damu.        

Bi.Asnath amewaeleza walengwa hao kuwa pamoja na changamoto hizo Mkoa wa Katavi umejiwekea mikakati mingi ikiwemo, Kuhakikisha shughuli za lishe zimepangwa katika mipango ya idara mbalimbali ambazo zinahusika na masuala ya lishe kama Afya, Elimu, Kilimo, maendeleo ya jamii na maji. Kuendelea kutoa chanjo kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 na matone ya vitamin ‘A’ na dawa za minyoo kwa akinamama wajawazito na watoto chini ya miaka 5. Kuhimiza kila mkazi wa eneo la halmashauri mwenye uwezo wa kufanya kazi kuwa na shamba kwa ajili ya kuzalisha mazao ya chakula, mazao ya biashara, mbogamboga na matunda kwa ajili ya kupunguza tatizo la upungufu wa chakula na umasikini wa kipato ngazi ya kaya. Kuhusu suala la usalama wa chakula Bi.Asnath amesema kuwa imezuka tabia ya wakulima kuuza mazao yao yakiwa shambani, hii ni hatari na jambo ambalo linatakiwa kukemewa kwa nguvu zote na kuwataka walengwa waliopo katika Mpango wa TASAF kuhakiksha kuwa wanahifadhi chakula.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved