• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BEVAC YAWEKA MSUKUMO MPYA KWENYE SEKTA YA UFUGAJI NYUKI NSIMBO.

Posted on: July 10th, 2025

Kwa kutambua mchango mkubwa wa nyuki katika uchumi wa jamii na utunzaji wa mazingira, Mradi wa BEVAC unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya kupitia shirika lisilo la kiserikali la Enabel, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, umeendesha ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Ziara hiyo iliyoongozwa na Mratibu wa Mradi, Bi. Flosia Vugo, imelenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha usindikaji wa mazao ya nyuki pamoja na kujionea jinsi wanachama wa Chama cha Ushirika cha Mazao ya Nyuki wanavyoendelea kuongeza thamani ya mazao yao kupitia mbinu bora na zenye tija.

Akizungumza katika ziara hiyo, Katibu wa chama, Bw. Peter Kalula, alieleza kuwa chama hicho kilianzishwa mwaka 2022 kikiwa na wanachama 80, lakini hadi Julai 2025, idadi hiyo imeongezeka hadi kufikia wanachama 170, wakiwemo wanaume 140 na wanawake 30. Ukuaji huo wa haraka ni kielelezo cha mwitikio chanya kutoka kwa jamii na uhalisia wa fursa zilizopo katika sekta ya nyuki.

Hata hivyo, Bw. Kalula alitaja changamoto zinazokikabili chama hicho, ikiwemo umbali wa ofisi za utoaji vibali, kupanda kwa gharama za vibali katika kipindi kifupi, na ukosefu wa masoko ya uhakika kwa mazao yao. Alitoa rai kwa Serikali na Mradi wa BEVAC kusaidia upatikanaji wa mikopo kupitia taasisi za kifedha na kuwezesha ufunguzi wa masoko ya kudumu kwa bidhaa za nyuki.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia Uchumi na Uzalishalishaji Mkoa wa Katavi, Bw. Kayumba Torokoko, aliwapongeza wanachama kwa usimamizi madhubuti wa ujenzi wa kituo hicho na akawahimiza kuendelea na ubunifu, ikiwa ni pamoja na kuanzisha vyanzo mbadala vya mapato ili kuimarisha shughuli zao za ufugaji nyuki.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bi. Christina Bunini, alikabidhi mizinga kwa wanachama wa chama hicho kama sehemu ya kusaidia jitihada za kuongeza uzalishaji, hatua inayoendana moja kwa moja na dhamira ya Mradi wa BEVAC ya kuimarisha miundombinu ya sekta ya nyuki na kuwawezesha wanavikundi kwa vitendea kazi muhimu.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved