• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

Posted on: May 20th, 2025

Katavi, Mei 20, 2025 — Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha mafunzo maalum ya siku mbili kwa Maafisa Utamaduni na Maafisa Biashara kutoka halmashauri zote za Mkoa wa Katavi, yakilenga kuwawezesha kutumia kwa ufanisi mifumo ya AMIS na TAUSI ambayo imeunganishwa kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa huduma kwa wasanii na wadau wa sekta ya sanaa.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa Masoko Mkuu wa BASATA, Bw. Martine Mwambene, amesisitiza umuhimu wa matumizi sahihi ya mifumo hiyo ya kidigitali ambayo inalenga kurahisisha usimamizi wa shughuli za sanaa, kurasimisha sekta hiyo, pamoja na kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri kupitia mikakati ya kisasa ya ukusanyaji.

“Mifumo ya AMIS na TAUSI ni nyenzo muhimu katika kuwasaidia maafisa wetu kuwahudumia wasanii, vikundi, taasisi, kampuni na wamiliki wa kumbi za burudani kwa ufanisi zaidi,” amesema Bw. Mwambene.


Kwa upande wake, Afisa Sanaa kutoka BASATA, Bw. Hassan Das, amehimiza maafisa hao kuhakikisha wanaratibu na kuwarasimisha wadau wote wa sanaa katika maeneo yao, hususan wamiliki wa miundombinu ya burudani kama kumbi za sherehe, starehe na maonyesho, kupitia mfumo wa AMIS.

Akitoa shukrani kwa niaba ya washiriki, Afisa Utamaduni wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bi. Tunele Eliya, amelipongeza BASATA kwa kuandaa mafunzo hayo, akieleza kuwa yamekuja wakati muafaka na yatawasaidia kuongeza ufanisi katika kusimamia shughuli za sanaa na biashara katika halmashauri zao.

Mafunzo hayo yamefanyika kuanzia Mei 19 hadi 20, 2025, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa BASATA wa kutoa elimu ya matumizi ya mifumo ya AMIS na TAUSI kwa maafisa wa serikali za mitaa kote nchini.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

    May 20, 2025
  • KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

    May 15, 2025
  • KATAVI YAZIDI KUNG'ARA UUZAJI WA KABONI

    May 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved