• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BARAZA MAALUM LA MADIWANI TANGANYIKA LAJADILI TAARIFA YA CAG, WATUMISHI WATAKIWA KUFUATA SHERIA.

Posted on: June 17th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, ametoa wito kwa watumishi wa umma kuhakikisha wanazingatia weredi na kufuata sheria katika utekelezaji wa majukumu yao, ili kuondoa hoja zisizo na mashiko katika ripoti za ukaguzi kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Ametoa angalizo kuhusu tabia ya baadhi ya watumishi kufanya kazi kwa mazoea, hali ambayo imekuwa ikisababisha hoja nyingi za ukaguzi.

Ameeleza kuwa hoja zinazojitokeza kutokana na uzembe na kutokuheshimu sheria, kama vile kufanya manunuzi bila kutumia risiti halali za EFD, zinaepukika kabisa iwapo watumishi watafuata sheria kikamilifu. Amehimiza kuwa wakuu wa idara wanapaswa kuwajibika moja kwa moja katika kujibu hoja hizo, hatua ambayo itasaidia kuondoa uzembe na kuboresha huduma kwa wananchi.

Katika baraza maalum la madiwani lililoketi leo Juni 17, 2025, kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, CPA Kasea Lyoba kutoka Ofisi ya CAG Amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imefanikiwa kupata hati safi ya ukaguzi kwa mwaka huo, ambapo jumla ya hoja 38 ziliibuliwa na mkaguzi. Kati ya hizo, hoja 18 zimehusu utendaji wa Halmashauri na 20 zimehusu usimamizi wa miradi ya maendeleo na mifuko mbalimbali. Aidha, hoja 16 kutoka miaka ya nyuma bado zimesalia, na hivyo kufanya jumla ya hoja zote kuwa 54.

Katika hatua ya utekelezaji, Menejimenti ya Halmashauri imeweza kutekeleza hoja 32 kati ya 54 kikamilifu na kupendekezwa kufungwa, huku hoja 22 zikiwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Akimhitimisha kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, Mhe. Hamad Mapengo, kwa niaba ya baraza la madiwani, ameushukuru uongozi wa mkoa pamoja na menejimenti ya halmashauri kwa ushirikiano mzuri uliowezesha utekelezaji mzuri wa majukumu katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BARAZA MAALUM LA MADIWANI TANGANYIKA LAJADILI TAARIFA YA CAG, WATUMISHI WATAKIWA KUFUATA SHERIA.

    June 17, 2025
  • RAS MSOVELA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO KWA KUTEKELEZA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE.

    June 19, 2025
  • MAADHIMISHO SIKU YA MTOTO AFRIKA, CHAGULAGA BADO NI KILIO KWA WASICHANA KATAVI.

    June 16, 2025
  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved