• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BARABARA ZABORESHA UCHUKUZI NA USAFIRISHAJI BIDHAA NA ABIRIA

Posted on: March 3rd, 2023

BARABARA ZABORESHA UCHUKUZI NA USAFIRISHAJI BIDHAA NA ABIRIA MKOANI KATAVI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko amesema uchukuzi wa bidhaa na usafirishaji wa abiria  umerahisishwa kwa wananchi ndani na nje ya Mkoa wa Katavi kutokana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanyika katika sekta ya miundombinu ya barabara katika mkoa huo.

Mhe. Mrindoko ameyasema hayo katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Mpanda uliopo Mjini Mpanda

Amesema Serikali yetu imeendelea kujenga barabara vijijini, kukarabati barabara na kukamilisha barabara mbali mbali, hivyo kuweka mazingira rahisi ya barabara kupitika muda wote kwa mwaka.

Mhe. Mrindoko amezitaja barabara za Vikonge na Stalike, Barabara za Mjini Mpanda, Barabara ya Mpanda-Tabora kuwa ujenzi wake umekamilika na kurahisisha uchukuzi wa bidha na usafirishaji wa abiria, hivyo kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi wa ndani na nje ya Mkoa wa Katavi.

Amesema ujenzi wa miradi mingine ya barabara unaendelea pia katika maeneo mbali mbali ya mkoa mfano Kibaoni-Stalike na Vikonge-Luhafe-Kigoma.

Hata hivyo kiongozi wa mkoa huyo amesikitishwa na vitendo vya wizi na uharibifu wa miundombinu ya barabara unaofanywa na baadhi ya wananchi wasiowaaminifu wanaoiba taa na nguzo za taa za barabarani.

Kufuatia uharibifu huo, Mhe. Mrindoko ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kuwakamata watu wote wanaojihusisha na wizi huo na kuwachukulia hatua za kisheria ili kukomesha tabia ya uharibifu ya miundombinu ya barabara.

Pamoja na juhudi zinazofanywa na Jeshi la Polisi mkoani Katavi, Mhe. Mrindoko amewataka pia wananchi wote wa Mkoa wa Katavi kulinda na kutunza miundombinui ya barabara ili iweze kuwanufaisha wananchi wa kizazi hiki na kijacho.

Umbali (kwa kilomita) wa mtandao wa barabara za umma za kitaifa na wilayani na vijijini umeendelea kuongezeka kila mwaka kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika miundombinu ya barabara na madaraja nchini.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC KATAVI AHADI MAZINGIRA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI

    March 09, 2023
  • RC KATAVI AWATAKA WANAWAKE KUSAMBAZA MAADILI MEMA KATIKA JAMII

    March 08, 2023
  • RC KATAVI ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOGUSWA NA MSIBA WA AJALI YA BASI

    March 07, 2023
  • UKATILI KWA WATOTO HAUKUBALIKI KWA MWENYEZI MUNGU

    March 05, 2023
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • MWENGE BLOG-KATAVI
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved