• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Bandari Karema yaanza Kazi.

Posted on: September 1st, 2022

Pichani:Moja kati ya Boti za Kitalii ilipotia nanga katika Bandari ya Karema mara baada ya Bandari hiyo kuanza kutumika 1 Septemba 2022.

Tanganyika -Katavi 

Wananchi na Wafanya biashara wasafirishaji wa bidhaa katika Mwambao wa ziwa Tanganyika wametakiwa kuachana na Bandari zisizo rasmi na badala yake kutumia Fursa ya Bandari ya kisasa ya Karema iliyoanza kutumika 1 Septemba 2022 kwa shughuli za kusafiri na Usafirishaji wa Bidhaa zao.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe.Onesmo Buswelu amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko ambapo 1 Septemba 2022 amefika katika Bandari ya Karema kushuhudia kuanza kwa shughuli za usafirishaji  Bandarini hapo.

Akizungumza  na Baadhi ya Wananchi Bandarini hapo DC Buswelu amewataka Wananchi na Wafanyabiashara wanaofanya shughuli za Usafirishaji katika mwambao wa Ziwa Tanganyika pamoja na Wananchi watakaosafiri kupitia Bandari mpya kutunza Miundombinu ya Bandari hiyo kusudi iweze kutoa huduma kwa muda mrefu zaidi.

Mhe.Buswelu ameitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA pamoja na Shirika la Uwakala wa Meli Nchini TASAC kushawishi Meli  kubwa kutoka Kongo na Maeneo mengine kutia nanga katika Bandari ya Karema.

Shabani Juma, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganganyika amemshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa Bandari hiyo ambapo ametoa rai kwa Wafanyabiashara wanaosafiri kwenda Kongo kutoka Dar es slaam na Maeneo mengine Nchini kutumia Barabara ya Tabora Mpanda iliyo katika kiwango cha Lami kurahisisha kufika kwa urahisi katika Badari ya Karema.

Naye Diwani wa Kata ya Karema Bw. Michael Kapata pamoja na shukrani alizozitoa  kwa Serikali amesisitiza juu ya umuhimu wa Ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha Lami kutoka Mpanda Karema ili kurahisisha shughuli za Uchukuzi na Usafirishaji wa Bidhaa kutoka Mpanda Mjini hadi Karema Bandarini.

Kaimu Meneja Mfawidhi wa bandari za TPA Ziwa Tanganyika Edward Mabula ameeleza kuwa Zaidi ya boti 4 za Abiria pamoja na Boti za Utalii zimewasili Bandarini hapo ambapo abiria 35 wamepokelewa katika Bandari hiyo wakitokea maeneo mbalimbali ya mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Bandari hiyo iliyogharimu Bilioni 47.9 ilihusisha ujenzi wa kivunja mawimbi, mlango bandari na gati ya meta 150 zenye uwezo wa kulaza meli zenye urefu wa meta 75 na upana wa meta 15, uchimbaji na uwekaji wa kina wa mlango wa bandari, jengo la ofisi, sebule ya abiria na shehena ya jumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved