• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Asasi zisizo za kiraia zaaswa kuzingatia Maadili ya Kitanzania

Posted on: September 12th, 2022

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko alipukutana na kuzungumza na Viongozi wa Asasi zisizo za kiserikali 12 Septemba katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda

Mpanda -Katavi. 

MKUU wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, amezitaka asasi zisizo za kiserikali (NGO), zisitumike kuharibu maadili na tamaduni za kitanzania, demokrasia, amani na uhuru wa nchi.

Mrindoko ameyasema hayo 12 Septemba 2022 katika kikao kilichokutanisha mashirika hayo, kilicholenga kujadili changamoto na maendeleo ya Mkoa wa Katavi, kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda ambapo amezisisitiza asasi hizo kuepuka  kutumika kisiasa na kuharibu maadili ya Kitanzania

Pia amezitaka taasisi hizo kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili katika mkoa huo, ikiwemo ubakaji, ulawiti na mimba za utotoni.

“Mkoa wetu wa Katavi matatizo hayo yanaendelea kutufedhehesha, masuala ya ubakaji na ulawiti yanaendelea kuongezeka, mimba na ndoa za utotoni, utoro shuleni, ajira za watoto, kazi za kingono, bado hamjaweza kufanya kazi zenu vizuri, hatujaona kama NGO zinazogusa maeneo hayo zinafanya kazi ya kutosha,” amesema na kuongeza:

“Mtoke na mkakati tunamalizaje suala hilo, suala hili si wajibu wa serikali peke yake na mashirika, hapa mmetaja kwamba mnayafanya masuala hayo, lakini kwa kweli bado yapo na yanaendelea kuongezeka na NGO mpo, shughuli zenu zinagusa hapo, je mnafanya wapi mambo haya mbona hatuoni matokeo? Amehoji RC Mrindoko.

Ameonya kuwa hatavumilia asasi yoyote, ambayo itabainika kuwa na lengo la kuchochea au kuhamasisha mapenzi ya jinsia moja na endapo itabainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Nae ofisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Katavi Willison Kennedy, amesema changamoto inayofanya mkoa huo kushindwa kutatua baadhi ya matatizo ni kutokana na kuwa na mashirika machache ya kimataifa, ambayo yanapokea ruzuku kutoka nje, huku akidai kuwa mashirika madogo yaliyopo ndani ya mkoa mengi hukosa ruzuku, kwa ajili ya kutelekeza miradi mbalimbali.

Mashirika hayo yamekutana kujadili mambo mbalimbali yanayo endelea katika Mkoa wa Katavi, kisha kutoka na ripoti ya pamoja na kwenda kuwasilisha katika mkutano wa kitaifa.


MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

 





 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved